Vic Sales Engine · Tanzania

Fuatilia Kila Lead
Hadi Alipie
Bila Kupoteza HATA mmoja..

Mfumo wa WhatsApp wenye follow-up za kiotomatiki na usimamizi wa wateja (CRM) — Uliotengenezwa Mahususi kwa biashara za Tanzania.

💬 Kukusanya Leads 🔁 Follow-Up za Otomatiki 💳 Malipo Rahisi Kwa Njia ya Malipo kwa simu na Benki 📊 Usimamizi wa Wateja

Zaidi ya Biashara 50+ Tanzania tayari zinatumia VIC SALES ENGINE kuongeza mauzo yao mara tatu zaidi bila kupoteza pesa wala muda.

vic-sales-engine.app — Dashibodi
Leads Leo
47
↑ +12 kutoka jana
Waliofuatiliwa
38
↑ 81% follow-up rate
Malipo Yaliyoingia
1.2M
TZS · Wiki hii
Kiwango Cha Kubadilika
34%
↑ +8% mwezi huu
Leads za Hivi Karibuni Hali
PM
Paul Masuka
+255 712 *** *** · Kanga
Mpya
EL
Eva Lugemarila
+255 754 *** *** · Nguo
Moto 🔥
KM
Khalifa Mkayuni
+255 768 *** *** · Chakula
Amelipa ✓
FI
Fatuma Issa
+255 789 *** *** · Dawa
Follow-up otomatiki imetumwa kwa leads 12 saa 2 zilizopita
Imetengenezwa Tanzania
Imeundwa Mahususi kwa mazingira ya biashara za hapa nyumbani.
Anza ndani ya Saa 24
Setup ya haraka. Hauhitaji hata kujua Teknolojia.
Malipo Rahisi. Haraka. Bila Usumbufu.
M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel Money na benki.
Msaada wa Masaa 24
Support ya moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Je, Biashara Yako bado Inapoteza Mauzo Kila kukicha?

Haya ndiyo matatizo unayokutana nayo kila siku kwenye biashara yako.

  • 😰 Leads zinapotea — Wateja Wanakutumia ujumbe WhatsApp. Hujibu kwa wakati. Mwisho Wanaenda kwa mshindani wako.
  • 🤦 Unasahau kufanya Follow-Up — Unasema utamfatilia mteja baadae. Messages zinaongezeka. Unamsahau.
  • 📊 Huna Takwimu za mauzo — Hujui nani aliulizia bidhaa au huduma zako. Nani alinunua. Wala wapi unapopotezea pesa.
  • Unapoteza Muda — Unatakiwa kufuatilia kila mtu peke yako. Lakini muda hautoshi. Unachoka.
73%
ya leads zinapotea kwa sababu ya kutofuatilia ndani ya saa 24 ya kwanza
Wateja wanaofuatiliwa mara 5 wana uwezekano mkubwa zaidi wa kununua
Suluhisho?
Vic Sales Engine inafanya follow-up otomatiki — wewe pumzika.

Kila Kitu Unachohitaji Ili uweze Kuuza Zaidi..

Zana zote ndani ya mfumo mmoja.

WhatsApp Lead Capture

Kila mteja anayekutafuta WhatsApp anaingia moja kwa moja kwenye mfumo. Haugusi chochote. Haupotezi hata mteja mmoja.

Follow-Up ya Otomatiki

Mfumo unamkumbusha mteja kwa wakati. Saa 1. Saa 24. Siku 3. Wewe unaendelea na kazi. Mfumo unafuatilia.

Ukusanyaji wa Malipo

Malipo yako yanaingia moja kwa moja. M-Pesa. Tigo Pesa. Airtel Money, au benki. Kila kitu kinakuwa kwenye dashibodi moja. Huchanganyikiwi tena.

Mini CRM Rahisi

Unaona kila hatua ya safari ya mteja wako. Historia yake. Hatua yake. Kama ni Mpya. Moto. Au Amelipa. Haubahatishi tena. Unajua nani wa kumfuatilia na kwa muda gani.

Ripoti za Mauzo

Unakuwa na hesabu za kweli za kila siku. Leads wangapi wameingia. Wangapi wamelipa. Wapi unapoteza mauzo. Data zote zinakuwa wazi. Hivyo inakusaidia kufanya Maamuzi sahihi.

Timu ya Mauzo

Unapata uthibiti wa wafanyakazi wako. Unaona nani anamfuatilia nani. Nani anauza zaidi. Kila kitu kinakuwa kiko wazi.

Anza kwa Hatua 3 Rahisi

Hauhitaji fundi wa IT. We Unaanza kutumia moja kwa moja.

Tutumie Ujumbe WhatsApp

Bonyeza kitufe cha “Pata Demo” na utuambie kidogo kuhusu biashara yako, na changamoto yako kubwa. Nasi tutakujibu ndani ya dakika 30 na kukuonyesha mfumo unavyofanya kazi,na jinsi utakavyokusaidia.

Setup Ndani ya Masaa 24

Timu yetu itatengeneza mfumo wako — ikijumuisha WhatsApp number yako, templates za ujumbe, na mtiririko wa follow-up kulingana na aina na changamoto ya biashara yako.

Angalia Mauzo Yakiongezeka

Leads zinanaswa. Mfumo unafuatilia. Malipo yanaingia. Wewe unafanya kitu kimoja tu — kufunga mauzo.

Biashara Zinazotumia Vic Sales Engine Zinaona Tofauti kubwa kwenye mauzo yao.

Ongezeko la Mauzo

Baada ya siku 30 mauzo yanaongezeka mara 3 zaidi. Follow-up haikatiki. Hakuna mteja anayesahaulika.

80%
Kupungua kwa Leads Zilizopotea

Asilimia 80 za Leads zilizokuwa zinapotea, sasa zinafika hatua ya malipo. Mfumo unawafuatilia hadi mwisho.

5h
Unaokoa Muda uliokuwa unapotea Kila Siku

Wafanyabiashara wanaotumia mfumo wetu wanashuhudia kuokoa wastani wa masaa 5 kila siku kwa sababu ya automation —na kupata muda zaidi kwa ajili ya mambo ya msingi ya biashara zao.

Gharama Yetu ni Nafuu na Iko Wazi

Lipa mara moja kwa setup, kisha kiwango kidogo kila mwezi. Hakuna ada zilizofichwa.

Ada ya Utengenezaji
150K–800K TZS

Mara moja tu · Inategemea ukubwa wa biashara

  • Utengenezaji kamili wa mfumo
  • WhatsApp Business API setup
  • Templates za follow-up (hadi 25)
  • Mafunzo ya timu yako
  • Uunganisho wa malipo (M-Pesa, CRDB n.k.)
  • Full Support ya wiki 2 ya kwanza
Anza Sasa →

ℹ️ Kumbuka: Bei hutegemea ukubwa wa biashara yako na idadi ya watumiaji. Wasiliana nasi kwa nukuu ya kibinafsi.

Wanasema Nini Wateja Wetu

Biashara za Tanzania zinaongelea matokeo halisi.

★★★★★
Kabla ya Vic Sales Engine nilikuwa napoteza leads nyingi kila siku. Sasa mfumo unafuatilia kila kitu bila mimi kuwepo na mauzo yameongezeka maradufu ndani ya miezi 2. Ninashangaa kwa nini haukuanza mapema!
Amina Mwenda
Muuzaji wa Nguo · Dar es Salaam
★★★★★
Nilikuwa ninafanya follow-up kwa mkono — inachukua muda mwingi na nasahau wateja wengi. Sasa kila lead anafuatiliwa kiotomatiki. Nimepata muda wa kufanya kazi muhimu zaidi kwenye biashara yangu.
Juma Kamau
Duka la Elektroniki · Arusha
★★★★★
Nilikuwa muoga mwanzoni, lakini baada ya wiki 3 za kutumia Vic Sales Engine niliona tofauti kubwa. Malipo yanaingia moja kwa moja, leads hazipotei, na team yangu inafanya kazi vizuri zaidi.
Fatuma Omar
Huduma za Afya · Mwanza

Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi

Je, ninahitaji simu yenye uwezo sana au kompyuta kubwa?
Hapana. Vic Sales Engine inafanya kazi kwenye simu yoyote ya Android au iPhone, na inaweza pia kutumika kwenye kompyuta yoyote yenye intaneti. Unachohitaji ni nambari ya WhatsApp Business tu.
Je, WhatsApp yangu ya kawaida itafanya kazi?
Tunapendekeza uwe na nambari ya WhatsApp Business iliyotengwa kwa ajili ya biashara, lakini tunaweza kukusaidia kuibadilisha. Nambari yako ya kawaida bado itafanya kazi — tutakuelekeza hatua kwa hatua.
Je, ninaweza kuacha kutumia mfumo nikitaka?
Ndiyo. Hakuna mkataba wa muda mrefu. Unalipa kwa mwezi, na unaweza kuacha wakati wowote. Tutakusaidia kupakua data zako kabla ya kuacha kutumia mfumo.
Je, taarifa zangu na za wateja wangu ziko salama?
Ndiyo, kabisa. Tumeweka hatua za usalama za hali ya juu — data zako hazishirikishwi na mtu yeyote. Pia tunafanya backup kila siku ili data zako zisipotee.
Ninaweza kuongeza wafanyakazi wangapi?
Mpango wa kawaida unajumuisha hadi watumiaji 3 (timu yako ya mauzo). Kama unahitaji nafasi zaidi, wasiliana nasi — tunaweza kubadilisha mpango kulingana na mahitaji yako bila tatizo.
Ninaweza kuona demo kabla ya kulipa?
Bila shaka! Bonyeza kitufe cha “Pata Demo WhatsApp” na tutakuonyesha mfumo wote unavyofanya kazi kwa video au demo ya moja kwa moja. Hakuna malipo ya demo.
🚀 Anza Leo

Acha Kupoteza Wateja.
Anza Kufuatilia na kuuza Kwa Akili.

Jiunge na biashara 50+ za Tanzania ambazo tayari zinaongeza mauzo yao kwa kutumia Vic Sales Engine. Demo ni bure, setup ni ndani ya masaa 24.
Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.